Journal matin

Habari za siku ya tano asubuhi 

  • Zaidi ya familia elfu mbili za wahami  kutoka Rutshuru na Nyiragongo, inayokuwa  kwenye nafasi Don Bosco Ngangi, walipokeya siku ya tatu  msaada wa chakula na vitu vingine uliotolewa na Kanisa la Methodiste Unie Kongo-Mashariki .
  • Jimboni Kivu ya Kaskazini, mapigano yaliripotiwa tena kati ya waasi wa M23 na wanajeshi wa FARDC siku ya inne  hii mchana katika eneo la Kibumba.
  • Katika jimbo la Ituri, shughuli za kiuchumi hazikuendeshwa leo hii siku ya inne katika vituo vingi vya ununuzi katika mtaani Irumu.
  • Kufuatana na wito huu  kutoka kwa jamii ya Yira ya kusimamisha  shughuli za kiuchumi, msimamizi wa mtaa wa  Irumu anatoa wito kwa wakaaji  kuendelea na shughuli zao kama kawaida.
  • Jimboni  Tanganyika,  wakaaji wa eneo la Moliro, katika mtaa wa Moba walishutumu siku ya tatu  uvamizi haramu wa sehemu ya inchi ya Kongo  na jeshi la Zambia.
  • Ukosefu wa usalama katika mtaa wa Kwamouth jimboni  Mai-Ndombe, mwanamke  aliuawa siku ya pili  iliyopita huko Kwamouth  na mwanajeshi wa FARDC ambaye alimpiga risasi
  • Jimboni Kivu ya Kusini, gereza kuu la Uvira linapata vifaa vipya vya kusaidia kulinda usalama ya wafungwa.
  • Kiongozi  wa Chuo Kikuu cha Kinshasa, Profesa Jean-Marie Kayembe alizindua siku ya inne vikao via kufasiriya azarani kazi ya utafiti  ku utaalam wa ikolojia ya magonjwa ya kuambukiza./sites/default/files/2022-11/181122-p-s-kinjournalswahilimatingraceamzati-00_web.mp3