Journal matin

Habari za siku ya inne asubuhi 

  • Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo haihusike na hatua yakutokununua  silaha.
  • Bunge la taifa  lilichaguwa  siku ya pili   azimio la kuizuia Serikali kuanzisha mazungumzo yoyote  na makundi yenyi kumiliki silaha ili kuwaingiza katika jeshi la serikali.
  • Chama cha Kisiasa kimachoongozwa na bwana Moise Katumbi kilitangaza siku ya pili  kuunga mkono  kwa wanajeshi wa FARDC ambao wanapigana katika mashariki mwa inchi.
  • Ukosefu wa usalama katika mtaa wa   Bagata, hasa katika sekta ya Wamba kufuatia ukatili unaofanywa na watu wasiojulikana wenye kumiliki silaha.  Msimamizi wa eneo hili ambaye ana wasiwasi, anajiuliza jinsi gani mchakato wa uchaguzi utafanyika katika eneo hili la jimbo la Kwilu.
  • Katika jimbo la Kasaï-Central , kunaripotiwa mzozo mkali  pa Bakua Bumba, sekta ya Mwanza-ngoma, katika mtaa  wa Demba.
  • Ugongwa wa Covid-19 uliongezeka kidogo kati ya mwisho wa mwezi wa kumi  na mwanzoni mwa mwezi huu wa kumi na moja  katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
  • Katika Jimbo la Tshopo, zaidi ya wafanyakazi mia nne na makumi mnane  wa offisi Kuu ya Mapato ya Tshopo wamepumuzishwa .
  • Waendesha pikipiki na madereva wa teksi na mabasi  wanakuwa tena wengi katikati ya mji wa Lubumbashi na wakisimama mahali popote hadi kufikia hatua ya kuzuia usafiri katika mji./sites/default/files/2022-11/101122-p-f-kinjournalswahilimatingraceamzati-00_web.mp3