Journal Soir

Habari za siku ya kwanza jioni tarehe 12/06/2023

  • Katika jimbo la  Ituri, yapata  watu makumi inne  na watano waliuawa na watu wenye silaha  usiku wa siku ya mungu  katika eneo la wakimbizi  la LALA karibu na kituo cha biashara cha BULE , karibu  kilomita mia moja kaskazini mwa Bunia katika mtaa wa Djugu.
  • Katika jimbo la  Kivu ya  Kaskazini, shambulio jipya lililohusishwa na waasi wa ADF usiku wa siku ya mungu  liliua watu wanane huko Kasindi, mji ulioko kilomita makumi mnane kutoka mji wa Beni.
  • Jimboni  Kasai, mashirika ya kiraia yamelaani hali ya  ukosefu wa usalama kwa mwezi mmoja sasa huko Tshikapa.
  • Jimbo la   Kivu ya Kusini linakumbwa na janga la kipindupindu kwa siku chache sasa.
  • Jimboni  Tanganyika, usimamizi wa kesi zinazoshukiwa za kipindupindu unaendelea katika eneo la afya la Kiambi, mtaani Manono.
  • Katika mtaa wa Beni, zaidi ya wakaaji  elfu kenda wa kijiji cha Samboko karibu kilomita makumi sita  kutoka Beni wamekosa  usaidizi wa kiafya kwa miaka mitano.
  • Ni lazma kupanda miti katika mji  wa Bukavu. Ni hivi ndivio  Waziri Gilbert Kabanda, akiwa moja wa wakuu wa mji huu, alisema kwa  wakazi wa Kivu ya Kusini, wakati ya mazungumzo yao./sites/default/files/2023-06/120623-p-s-journalswahilisoirgraceamzati-00_web.mp3