Journal matin

Habari za siku ya tatu asubuhi 

  • Liwali wa jimbo la Kivu ya Kaskazini anatoa wito kwa wakaaji wa Goma kutulia na kuwa waangalifu.
  • Katika Jimbo hilo la Kivu ya Kasakazini, upatikanaji wa maji ya kunywa ni hitaji kubwa ya wahami .
  • Katika jimbo la  Kwilu, hali ya maisha ya wahami  ni mbaya  katika  mtaa wa  Bagata.
  • Jimboni  Kwilu,  kunaonekana  siku hizi ukosefu ya mazao ya kilimo na kusababisha ongezeko la bei ya bizaa hiyo kama mahindi na mihogo  mjini Kikwit.
  • Mtaa wa  Lubudi jimboni Lualaba haina umeme kwa muda wa miezi miwili. Matokeo yake ni kwamba shughuli za kibiashara haziendeshwa vizuri.
  • Jimboni Kasai ya mashariki,chama cha kifeza cha wanawake wa Afrika mjini Mbujimayi, MUFFA kwa kifupi,  kilipewa jana siku ya pili  dola laki moja, kutoka kwa shirika   Kemesha, ambao inakutanisha mashirika mengine ikiwemo shirika Widal, Pierrette Bemba, Suzane Tshimwanga , MUFFA Mbuji Mayi mbele ya wanawake kadhaa wanamemba wa chama hicho.
  • Jimboni Maniema, mkurugenzi jimboni ahusikaye na  elimu ya  Maniema ya kwanza  anaendelea na  kampeni yake ya  kupiganisha matendo mabaya  katika shule ya jimbo hilo./sites/default/files/2022-11/161122-p-s-kinjournalswahilimatingraceamzati-00_web.mp3