Journal Soir

Habari za siku ya pili jioni tarehe 20/06/2023

  • Mpinzani Franck Diongo, kiongozi  wa chama cha kisiasa cha Mouvement Lumumbiste Progressive, MLP kwa kifupi , alikamtwa  siku ya pili hii  asubuhi na watu wenye silaha waliovalia vazi na kijeshi  katika makutano ya barabara za Kabinda na Huilleries hapa mjini Kinshasa.
  • Marekani inakaribisha ripoti ya mwisho ya  Wataalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
  • Jimboni Ituri, shirika ya kiraia linaomba haki ya kijeshi kutoa hati za kukamatwa kwa wahusika wote wa uhalifu uliofanywa katika jimbo hili.
  •  "Endelea kutumaini kuishi ingawa mbali na nyumbani". Huu ndio ujumbe uliotumwa kwa wakimbizi wanaoishi  mjini Goma na mwanamke mjasiriamali wa Kongo.
  • Ulimwengu unasherehe siku ya pili hii, Siku kuu ya Wakimbizi. Huko jimboni Kivu ya Kusini, asilimia makumi kenda  na sita ya wakimbizi wa Burundi katika jimbo hili, yaani zaidi ya watu elfu makumi inne wanapatikana katika eneo la Fizi pamoja na karibu ya waomba hifazi elfu tatu wa Burundi.
  • Kulianzishwa siku ya kwanza huko Zongo katika jimbo la  Kongo Central  kikoa cha  utetezi na mazungumzo  juu yakupiganisha rushwa pamoja na na kuhusu kuboreshwa  kwa sekta ya sheriya.
  • Katika Jimbo la Kwilu, CENI inasema iko tayari kwa shughuli ya mapokezi ya  wagombea wa ubunge  kuanza tarehe makumi mbili na tano mwezio huu wa sita.
  • Ilizinduliwa mnamo tarehe makumi mbilio mwezi wa sita , mwaka elfu moja miye kenda na makumi mnane na tatu  na Rais wa zamani Mobutu, daraja iiitwao Pont Maréchal , huko Matadi, ilieneza  miaka mwaka makumi inne siku ya pili hiii./sites/default/files/2023-06/200623-p-s-kinjournalswahilisoirgraceamzati-00_web.mp3