Journal Soir

Habari za siku ya inne asubuhi tarehe 15/06/2023

  • Kulifunguliwa jana mjini Lubumbashi  kikao cha kumi na  nane DRC Mining Week, yani wiki  ya madini inchi Kongo yakidemokratia. Mada ni "Tambua  ushindi wa sekta ya madini nchini DRC "
  • Jimboni Kivu ya Kusini, Shirika  ya kiraia inaelezea wasiwasi wake kuhusu  kazi ya mradi ya maendeleo ya mitaa  mia moja na makumi inne na tano katika jimbo hilo.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kusini, visa vingi vya nyumba kuwaka moto  katika mji la Bukavu si vya uhalifu  lakini ni kwa kutokuwa makini .
  • Katika mji wa Goma,  mwanabunge Prince Kihangi anamuomba liwali wa jimbo kusimamisha  kazi ya ujenzi  ya  uzio wa gereza kuu la Munzenze.
  • Daktari  kiongozi wa Kituo cha Usambazaji Damu mjini  Butembo anaalika watu wa moyo mwema kutoa damu yao ili kuokowa maisha ya wengine.
  • Na mjini Beni, watu watano watoaji bora wa damu kwa miaka mengi,  walipewa vieti na  heshima  siku ya tatu hii  katika sherehe ya Siku kuu ya Wachangia Damu Duniani.
  • Katibu Mkuu makamu  wa Umoja wa Mataifa anayehusika na  suala la ubakaji  unaofanywa wakati wa migogoro anayepatiakna  mjini Goma tangu siku ya pili, alitembelea siku ya pili hiyo , Hospitali ya Heal Africa mjini Goma.
  • Muungano wa kitaifa wa vyama vinavyopigana dhidi ya mimba zisizotamaniwa  unaomba kuondowa adhabu  kuhusu jambo la kuondowa  mimba nchini kongo ya kidemokratia kufuatana  wa azimio ya Maputo.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kaskazini: mwanamke ambaye alishtakiwa  kuua mtoto, alihukumiwa kwa azabu ya kifo siku ya pili na mahakama ya kijeshi ya mji wa Goma./sites/default/files/2023-06/15062023-p-s-journalswahilimatingraceamzati-00_web_.mp3