Journal matin

Habari za siku ya kwanza asubuhi ya tarehe 19/06/2023

  • Jeshi la Uganda linatoa wito kwa wakazi wa Bwera kuwa waangalifu na kushutumu adui yoyote katika maeneo yao.
  • Baada ya shambulio hili la waasi  wa ADF, wa shule katika eneo la  Uganda jirani na mji wa Kasindi wa Kongo Ya Kidemokratia, wanajeshi wa FARDC wanasema wako waangalifu  kwa ajili ya usalama wa mji huu wa mpakani na wakazi wake.
  • Lawama na kushutumu  shambulio  hili la waasi wa  ADF kwenye shule nchini Uganda zanatoka kote ulimwenguni.
  • Jimboni Ituri, majaribio kadhaa ya mashambulizi ya makundi yenye kumiliki  silaha yalizuiwa  wiki iliyopita  na  jeshi la Monusco katika mtaa wa  Djugu.
  • Katika jimbo la Ituri tuwajulishe kwamba, zaidi ya watu elfu kumi na mbili wahami  walipokeya wiki inayopita  msaada wa vifaa vya nyumbani katika maeneo ya  Mwanga na Kunda, karibu  kilomita kumi kaskazini mwa Bunia.
  • Rais Félix-Antoine Tshisekedi alielezea wasiwasi wake kufuatia kuzorota kwa hali ya kuunda biashara katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
  • Miezi sita kabla ya uchaguzi, , Rais wa zamani Joseph Kabila baada ya kimya kwa muda mrefu  anaanza mawasiliano na wanamemba wa chama chake cha  kisiasa.
  • Katika jimbo la Kivu ya Kaskazini, wafanyabiashara wa  mafuta,  wanakubaliana tena juu ya malipo  wa ushuru wa kawaida wa ujenzi katika jimbo hilo./sites/default/files/2023-06/190623-journalswahilimatingraceamzati-00_web_.mp3